Monday, March 24, 2025

MASWALI YANAYOWEZA KUULIZWA KWENYE INTERVIEW YA TRA MARCH 2025

 

ANGALIZO

Haya ni baadhi ya mawaswali  ambayo yanaweza yakatoka au yasitoke kutokana na ajira ulioiomba, hiyo unatakiwa kuyapitia na kusoma kisha fanyia utafiti mtandaoni na kuwauliza marafiki unaowajua ambao walibahatika kufanya hizo interview, nakutakia kila laheri kwenye interview yako. Mwenyezi mungu awe na wewe.

 

LINK ZA MASWALI


CUSTOMS ASSISTANT II INTERVIEW POSSIBLE QUESTIONS AND ANSWERS


Customs Officer II TRA


Public Relations Officer

Friday, February 19, 2021

James Giblin A History Of The Excluded: making family a refuge from state in twentieth-century Tanzania

 

Author/Creator
Giblin, James Leonard.
Contributor
Giblin, Blandina Kaduma.   

Download book From the following links below

- https://www.researchgate.net/publication/30430163_Giblin_J_L_-_A_History_of_the_Excluded_Making_The_Family_a_Refuge_from_the_State_on_Twentieth-Century_Tanzania

- https://uneasterq.firebaseapp.com/aa944/a-history-of-the-excluded-making-family-a-refuge-from-state-in-twentieth-century-tanzania-eastern-african-studies-by-james-l-giblin-0821416685.pdf

-https://www.amazon.com/History-Excluded-Twentieth-Century-Tanzania-Eastern/dp/0821416693

-

Tuesday, February 2, 2021

Tomb Raider 2018


"Baada  ya  Maelezo  ya  Richard Croft"



Kufuatia kwa  kutoweka kwa baba yake, Richard Croft (Dominic West), Lara Croft (Alicia Vikander) mrithi  wa  mali  na  kampuni  za  baba yake,  anaishi  kama  masikini kwa  kutotegemea  mali  za  baba  yake aliyemuacha  akiwa  mdogo  miaka  7  iliyopita, akiwa  na  hasira  Kutokana  na  baba  yake kuondoka  bila  kusema  chochote. Lara  anaishi kiubishi  siku  hadi  siku  kwa  kufanya  kazi  mbali mbali (kama special delivery  na  n.k). 

Siku  moja  baaada  ya  kumaliza  kudeliver  mizigo  yake  na  baiskeli,  anapitia  gym  na  kukuta  marafiki  wakiungumzia  bet.lara anakua  interested  na  hiyo  bet  kwakua  anahitaji pesa,  so  marafiki  wanampa  mashart  ya  bet,  kwamba  ili  aweze  kushinda  pesa  anihitaj kufunga  mkia  wa  fox  nyuma  ya  baiskel  yake  na  kukimbia mpaka  atakapofika  mtaa  wa  pili  akiwa  kwenye  hiyo  race  lara  anamuona  mtu  anayefanana  na baba yake  hivyo  anajikuta  akiwa  amesababisha  ajali kwa  kugonga  gar  ya  polisi.Wakati yeye amekamatwa baada ya ajali ya baiskeli inayohusisha gari la polisi,  mshirika wa biashara wa Richard Ana Miller anamuwekea dhamana na anamwambia kwamba ikiwa hatadai urithi wake, na  kusaini  docs  za  kuhalalishwa yeye  kuwa  mridhi  na  msimamizi   wa  mali za baba yake ..... Basi  atakosa  kila  kitu  ikiwemo   nyumba  na  makampuni  yake  yatauzwa.

Lara anakubali na  anakwenda  kwenye  offisi  ya baba  yake  kusaini  docs  ambapo anakutana  na  Ana Miller  na  mwanasheria  wa  baba  yake.  Lara  anahofu  kuwa  kama atasaini  itamaananisha  kuwa  baba  yake  amekufa  kweli. Wakati  anajifikiria  kusaini  mwanashera  anampa sanduku la puzzle la Karakuri ambalo limeachwa na baba yake, ambalo linaongoza kwenye chumba cha siri katika kaburi la baba yake. Huko anapata ujumbe wa video kabla ya kumbukumbu kutoka kwa Richard maelezo yake ya utafiti katika Himiko, Malkia wa kihistoria wa Yamatai ambaye alisema amri ya nguvu juu ya maisha na kifo. Richard anaonya Lara kuharibu utafiti wake wote lakini Lara anaamua si hivyo apate kuchunguza zaidi, kwani  anahitaji  kujua ni  nini  kilichomkuta  baba  yake.

Lara anaamua  kwenda Hong Kong ambako ambapo  ndipo  ujumbe  unaonesha  baba  yake  alipo  kwenda,  huko  anamuajiri Lu Ren (ALIYECHEZA  SERIES  ZA INTO  THE  BADLANDS), nahodha wa Endurance, kuelekea Bahari ya Ibilisi hadi kisiwa cha Yamatai. Akiwa  safarini Meli yao  inapigwa na  dhoruba kali na Lara anatupwa pwani ambako yeye anapoteza fahamu. Lara  anaamshwa  na  Mathias Vogel, kiongozi wa safari anayetafuta kaburi la Himiko. 

Safari hiyo imesaidiwa na shirika la kivuli lililoitwa Utatu ambalo linajaribu kuunganisha na silaha (nguvu) za Himiko. Vogel anamshukuru lara  kwa  kumletea  reseach  za baba  yake  kisha  anamchukua  kama mfungwa, na  kumwambia  Lara  kuwa  yeye  ndiye aliyemuua baba yake na anatarajia kutumia utafiti wa Richard ili kuendelea safari yake  ya  kutafuta  kaburi  la  Himiko.

ENDELEA


zaidi kuhusu movie 


Directed by Roar Uthaug

Produced by Graham King

Screenplay by Geneva Robertson-Dworet, Alastair Siddons

Story by Evan Daugherty, Geneva Robertson-Dworet

Based on Tomb Raider by Crystal Dynamics


Starring Alicia Vikander

               Dominic West

               Walton Goggins

               Daniel Wu

               Kristin Scott Thomas

Music by Tom Holkenborg

Cinematography George Richmond

Edited by Stuart Baird, Michael Tronick

Production companies Metro-Goldwyn-Mayer, Warner Bros. Pictures, GK Films, Square Enix

Distributed by Warner Bros. Pictures

Release date - March 2, 2018 (Berlin)

                            March 14, 2018 (United Kingdom)

                            March 16, 2018 (United States)

Running time 118 minutes

Country      - United Kingdom

                       United States

Language English

Budget $90–106 million

Box office $274.7 million


                    for  more  movies contact


By:Gualbert Kashasha  

   +255 623 352 792


Saturday, July 18, 2020

JINSI YA KUHIFADHI VITU VYAKO KWENYE GOOGLE DRIVE


Hello, leo  nitawaonesha jinsi ya kuhifadhi/ficha vitu vyako kwenye GOOGLE DRIVE kwenye simu yako. 

KWA  UFUPI
GOOGLE DRIVE ni huduma ya uhifadhi wa faili na maingiliano iliyoundwa na Google. Ilizinduliwa Aprili 24, 2012, Hifadhi ya Google inaruhusu watumiaji kuhifadhi faili kwenye seva zao,  kwa  upande  wa  simu  inaweza  tumika  kwenye  simu  aina  ya  Android na iOS unaweza  tumia  kuhifadhi  vitu  mbalimbali  zenye  format  aina  zote  (MFANO picha, video. Pdf, ms, software, vyeti, hati za nyumba na vituvingine vyovyote ambavyo ni private). 

GOOGLE DRIVE  hutoa gigabytes 15 za uhifadhi wa bure kupitia Google One. Google One pia hutoa gigabytes 100, gigabytes 200, terabytes 2, terabytes 10, terabytes 20, na terabytes 30 zinazotolewa kupitia mipango ya kulipwa kwa hiari. Faili zilizopakiwa zinaweza kuwa ukubwa wa hadi 5 terabyites kwa ukubwa.

JINSI YA KUTUMIA
Unachotakiwa  kufanya  ni  kufuata  hizi  hatua  zifuatazo:

HATUA  YA  KWANZA
Nenda  kwenye  menyu  ya  simu  yako  ufungue  DRIVE,  Kama  haipo  inabidi  ui-install  kwenye  google  play  store.



HATUA YA  PILI
Itafunguka  Hivi  kama uonvyo hapo chini

HATUA  YA  TATU
Hakikisha  email  yako  inasoma kwenye DRIVE kama  hakuna  angalia  duara  mkono  wa  kushoto  kisha ubonyeze kuhakiki au  angalia  mkono  wa  kulia  uangalie  kama  itaonekana  picha  uliyosave  kwenye  profile  ya  email  yako  au  herufi  ya  jina  lako.




HATUA  YA  NNE
Hakiki  storage  yako,  kumbuka  google  wanakupa  GB15  za  kutumia  bure,  ukitaka  kuongeza  zaidi  inabidi  ulipie  ila  so  far  hakuna  mtu  anayezifkia  hizo  kwa  matumizi  ya  simu. 



HATUA  YA  TANO
JINSI  YA  KU-UPLOAD  KITU  KWENYE  DRIVE, bonyeza  ala  ya  kujumlisha (ili kuadd ADD)



HATUA YA SITA
Baada  ya  kubonyeza  +  zitatoka option  tofauti  zote ni muhimu ila leo  tunaangalia jinsi ya ku-upload kitu  ambacho  tiyali  kipo  kwenye  simu,  hivyo  ili  kuingiza na kuhifadhi inabidi  ubonyeze  upload (option iliyozungushiwa  duara hapo chini)



 HATUA YA SABA
Itakupeleka  kwenye  vitu  ambavyo  umetumia muda sio  mrefu  (RECENT) kama  picha  unayotaka  kuiupload  haionekani  hapa  unatakiwa  kubonyeza  hilo  duara  mkono  wa  kushoto  pembeni mwa  neno RECENT.

HATUA YA NANE
Itakupeleka  kwenye  source  ya  mafaili  yako  kila  simu  ipo  tofauti  ila  baadhi  ya  vitu  vipo  sawa  so,  mfano  unataka  kuupload  picha.  Unakwenda  kwenye  IMAGES


HATUA  YA  TISA
Picha  ninayotaka  kui-upload  ipo  kwenye  folder la bluetooth


HATUA  YA  KUMI
Chagua  picha utakayo





HATUA YA  KUMI NA MOJA
Ukiipata  ibonyeze  kwa  nguvu  mpaka  itokee  tiki  then nenda  kulia  kwako utaona neno  OPEN ibonyeze  ili  ianze  ku-up-load





HATUA YA KUMI NA MOJA
Baada  ya  kuopen Itatokea  hivi, bonyeza  ALLOW  ili  kuruhusu  DRIVE  kupata  access  ya  mafaili  ya  simu  yako






HATUA  YA  KUMI  NA  MBILI

Baada  ya  hapo  itaanza  ku-upload.  MUHIMU kila  simu  inasetting  tofauti  so  inategemea  simu  yako  umeiset  vipi  kwenye  network,  simu  nyingine  zina-upload  moja  kwa moja  nyingine  mpaka  ubonyeze  neno  RESUME  kama  ionekanavyo  hapo  chini. 



HATUA  YA  KUMI  NA  TATU
Baada  ya  hatua  ya  12  kukamilika  picha  yako  itaupload  kwenye  DRIVE.  Hivyo  unamaamuzi  ya  kuifuta  picha  original  iliyopo  kwenye  simu  au  kuicha  kwani  ikiwa  kwenye  DRIVE  inakaa  huko  mpaka  utakapo  amua  wewe  kuifuta 







NJIA  YA  PILI  YA  JINSI  YA  KUHIFADHI  AU  KUFICHA  VITU  KWAKO  KWENYE  GMAIL 


1.  FUNGUA  GALLARY  AU  GOOGLE PHOTOS
     chagua  picha  utakayo  kuiweka  kwenye  GOOGLE DRIVE ibonyeze  kwa  nguvu  then           share  kwenye  Drive (fanya  kama  unavyofanya  unapomrushia  mtu  kitu  kwenye                     Bluetooth  )


2. CHAGUA  KUSHARE  KWENYE  DRIVE  kama ioneshavyo  hapo  chini



3. ITAFUNGUKA  HIVI utaamua  wewe  mwenyewe  kuirename  au  kuiacha  kama  ilivyo  kisha          bonyeza  SAVE




4. ITAFUNGUKA  HIVI  UTABONYEZA  RESUME



5. UNAKUA  UMEMALIZA  THEN  ITAANZA  KU-UPLOAD



6. IKIMALIZA  KULOAD  PICHA  INAKUA  IMEKAA  KWENYE DRIVE



DONE

Hatua  hizi  unaweza  zifanya  kwa  mafaili  ya  aina  yote  utakayo  na  yanakua  salama so  hata  ikitokea  umepoteza  simu  yako  au umepoteza  hard copy  ya  vitu  vyako  bado  unakua  na  backup  ya  data  zako  muhimu  kwenye  DRIVE  bila  tatizo  lolote


Tuesday, June 9, 2020

MARRY’S FORGIVENESS pt1



JE WEWE UNGEFANYA NINI?
       Mzee  John Charles Kayumba  alibarikiwa  na Mungu, ujanani mwake Mungu alimbariki akapata mke mwema  aitwaye Rose Jamini , wote walikuwa ni wachamungu, kama walivyo wanandoa wengine wa zamani walipitia mengi katika maisha yao ya ndoa shida na raha, lakini walivumilia na mpaka Mungu akawajalia kupata watoto wanne, wakiume  watatu na msichana mmoja. (Charles, Emilianna, Makuda na Mussa). Mzee huyo alikuwa ni mtumishi serikalini na mkewe huyo alikuwa ni mama wa nyumbani anayeendesha biashara ndogondogo. Maisha yaliendelea, walilea watoto wao na kuishi kwa furaha sana. Miaka ilipita wakabarikiwa kujenga nyumba tatu, ambapo nyumba moja waliishi wao na watoto wao na nyingine walipangisha.

          Siku moja ilikuja kugundulika kuwa mzee huyo alizaa mtoto mwingine nje ya ndoa. Mkewe alihuzunika na kuumia sana, Baada ya mkewe kupata habari hizo kutoka kwa majirani, alifanya uchunguzi na kugundua kuwa habari hizo ni za kweli, na nikweli mzee huyo alizaa mtoto wa kike na mwanamke mwingine. Siku  moja  baada  ya  kupata  na  kukamilisha  upelelezi wake na kupata uhakika alimsubiri mumewe na kumuuliza, Mumewe alikiri na kukubali jambo hilo. Jambo hilo lilileta mvurugano kwenye ndoa yao kiasi kwamba ililazimu kuitwa wazazi na  ndugu  wa pande zote mbili pamoja na viongozi  kathaa wa dini ili waje kulisuluhuisha, kikao  kilikua  kikubwa na kirefu sana  ila  Mungu ni mkubwa, maana aliwezesha usuluhuisho huo kuwa wa amani na Yule mke kumsamehe mumewe,  wageni walioalikwa kwenye kikao hicho waliamuru  mume arudi kwenye ndoa na aachane na huyo mwanamke mwingine.

        Miezi kadhaa ilipita mke wa  Mzee John alimuomba mumewe amlete huyo mtoto aje kukaa nyumbani kwao na kumlea pamoja na wenzake, mzee John alifurahi sana kwani aliona ni jambo bora watoto wake wakikua pamoja wakitambuana na kupendana kama ndugu.  Kweli Yule mtoto alikuja nyumbani hapo na kulelewa na mama huyo, Alikua anaitwa Mary, alisomeshwa na kuishi hapo kipindi chote hadi alipomwaliza shule ya msingi, Mungu alimjalia kwani alifaulu mtiani wake na kuendelea na elimu ya sekondali. Kipindi yupo kidato cha pili Mzee John (baba yake) alifariki. Ilikua  ni  pigo  kubwa  kwenye  familia  hiyo, mazishi  yalifanyika. Ilipofika siku ya mirathi Mama na Ndugu zake Mary ( dada na kaka zake pamoja na mama yake aliyekuwa anamlea ) walimkataa na kumwambia kuwa hawamtambui, mama  mjane alitoa  maelezo kwenye kikao hicho kuwa binti huyo alikua ni  mfanyakazi wao wa ndani na waliamua kumlea na kumsomesha kama mwanafamiia ila sio mtoto halali wa mwarehemu mumewe na inatakiwa aondoke arudi kwao, Binti Yule hakuamini kinachomtoka  kinywani mama yake huyo aliangua kilio na kuuliza kama kunakitu amekosea hadi leo amkatae, alihuzunika sana na kuamua kuondoka na kurudi kwa mama yake mzazi.

      Maisha  ya  mama  yake  yalikua  ya  kimaskini  sana. Alimpokea  mwanae na  kuishinae  hapo.  Ingawa  alikua  bado  anasoma  hakuwa na budi kumsaidia  mama yake  baadhi  ya  shughuli  ili waweze kupata  kipato,  siku za kawaida baada ya kurudi  shule alikua anakwenda mgahawani kwa  mama  yake  na  kumsaidia  kazi,  alipata  usumbufu  mwingi  kutoka  kwa  wateja  wa  kiume  ambao  mara  nyingi  walikua  wakimtongoza  na  kumtaka  kimapenzi. Kutokana na malezi  aliyopewe na heshima aliliokuwa nayo  alijitahidi  kudharau usumbufu  huo  ila  ulivyoukua unazidi alibidi awe mkali.  Mama  yake  alimsihi  asiwe mkali kwa wateja  kwani  akifanya  hivyo  watamkimbia  mgahawani  kwake  na  ukiangalia  tangu  yeye  arudi  wateja  wamekua  wengi,  alimwambia  anachotakiwa  kufanya  ni  kuwasikiliza  ila  asifanye  au  kukubali  watakavyo.  Alifanya  hiyo  ila  kadri  siku  ziendavyo  vishawishi  vilizidi  kuwa  vingi  shuleni  na  nyumbani, kwani  hata  baadhi  ya  waalimu  nao  walikua  wanamtaka.  Akajikuta  anahongwa  na  wateja,  wengine  kumuachia  hela  kubwa  wakidai  ni  zawadi.  Mary aliangalia  maisha ya marafiki zake shuleni  wengi  wanavaa vizuri na  wengine wanamiliki  hadi  simu.  Mary  bado  akapiga  moyo  konde  na  kubaki  kwenye  mstari.

     Siku  moja  wakati  anatoka  shule  alisikia  mlio  wa  honi  ya  pikipiki,  alipogeuka  nyuma  alikuta  ni  teacher  wake,  teacher  alimuomba  ampe  lifti  Mary hakua  na  shaka  kwakua  alijua  mwalimu  anapitaga  njia  moja  ya  nyumbani  kwao,  alipanda  pikipiki  huku  teacher  akimpa  pole  kwa  kutembea  umbali  mrefu.  Njiani  teacher  alimuomba  apitie  nyumbani  kwake  kwanza abadili  nguo  kisha  ampeleke  mpaka  kwao.  Mary  alikubali,  walipofika  nyumbani  kwa  teacher  mary  alibaki  nje  Teacher  akaingia  ndani kubadili  nguo,  kipindi  yupo  nje  alishangaa  anaitwa  na  teacher  aingie  ndani,  mary  alijibu  hawezi  kwani  anaharaka  kurudi  akamsaidie  mama  yake,  Teacher aliendelea  kumuomba  aingie  ili  amsaidie  kusahihisha  mitihani, Mary  aliomba aende anaogopa  mama  atamgomba  kama  akichelewa, Teacher  alimwambia anamitihani michache tu hivyo amsaidie fasta ili amuwahishe, Mary alimuomba basi aitoe nje ila teacher  akamwambia  nje  watu wakiona  watahisi  vibaya.  Basi  Mary  akajikuata  anakubali,  aliingia  ndani  na  kukuta  mitihani  ipo  mezani  marry  alikaribishwa  kwenye  kochi  akaaanza  kusahisha,
 End  of  part  one

MASWALI YANAYOWEZA KUULIZWA KWENYE INTERVIEW YA TRA MARCH 2025

  ANGALIZO Haya ni baadhi ya mawaswali  ambayo yanaweza yakatoka au yasitoke kutokana na ajira ulioiomba, hiyo unatakiwa kuyapitia na kuso...