JE WEWE UNGEFANYA NINI?
Mzee John Charles Kayumba alibarikiwa na Mungu, ujanani mwake Mungu alimbariki akapata mke mwema aitwaye Rose Jamini , wote walikuwa ni wachamungu, kama walivyo wanandoa wengine wa zamani walipitia mengi katika maisha yao ya ndoa shida na raha, lakini walivumilia na mpaka Mungu akawajalia kupata watoto wanne, wakiume watatu na msichana mmoja. (Charles, Emilianna, Makuda na Mussa). Mzee huyo alikuwa ni mtumishi serikalini na mkewe huyo alikuwa ni mama wa nyumbani anayeendesha biashara ndogondogo. Maisha yaliendelea, walilea watoto wao na kuishi kwa furaha sana. Miaka ilipita wakabarikiwa kujenga nyumba tatu, ambapo nyumba moja waliishi wao na watoto wao na nyingine walipangisha.
Siku moja ilikuja kugundulika kuwa mzee huyo alizaa mtoto mwingine nje ya ndoa. Mkewe alihuzunika na kuumia sana, Baada ya mkewe kupata habari hizo kutoka kwa majirani, alifanya uchunguzi na kugundua kuwa habari hizo ni za kweli, na nikweli mzee huyo alizaa mtoto wa kike na mwanamke mwingine. Siku moja baada ya kupata na kukamilisha upelelezi wake na kupata uhakika alimsubiri mumewe na kumuuliza, Mumewe alikiri na kukubali jambo hilo. Jambo hilo lilileta mvurugano kwenye ndoa yao kiasi kwamba ililazimu kuitwa wazazi na ndugu wa pande zote mbili pamoja na viongozi kathaa wa dini ili waje kulisuluhuisha, kikao kilikua kikubwa na kirefu sana ila Mungu ni mkubwa, maana aliwezesha usuluhuisho huo kuwa wa amani na Yule mke kumsamehe mumewe, wageni walioalikwa kwenye kikao hicho waliamuru mume arudi kwenye ndoa na aachane na huyo mwanamke mwingine.
Miezi kadhaa ilipita mke wa Mzee John alimuomba mumewe amlete huyo mtoto aje kukaa nyumbani kwao na kumlea pamoja na wenzake, mzee John alifurahi sana kwani aliona ni jambo bora watoto wake wakikua pamoja wakitambuana na kupendana kama ndugu. Kweli Yule mtoto alikuja nyumbani hapo na kulelewa na mama huyo, Alikua anaitwa Mary, alisomeshwa na kuishi hapo kipindi chote hadi alipomwaliza shule ya msingi, Mungu alimjalia kwani alifaulu mtiani wake na kuendelea na elimu ya sekondali. Kipindi yupo kidato cha pili Mzee John (baba yake) alifariki. Ilikua ni pigo kubwa kwenye familia hiyo, mazishi yalifanyika. Ilipofika siku ya mirathi Mama na Ndugu zake Mary ( dada na kaka zake pamoja na mama yake aliyekuwa anamlea ) walimkataa na kumwambia kuwa hawamtambui, mama mjane alitoa maelezo kwenye kikao hicho kuwa binti huyo alikua ni mfanyakazi wao wa ndani na waliamua kumlea na kumsomesha kama mwanafamiia ila sio mtoto halali wa mwarehemu mumewe na inatakiwa aondoke arudi kwao, Binti Yule hakuamini kinachomtoka kinywani mama yake huyo aliangua kilio na kuuliza kama kunakitu amekosea hadi leo amkatae, alihuzunika sana na kuamua kuondoka na kurudi kwa mama yake mzazi.
Maisha ya mama yake yalikua ya kimaskini sana. Alimpokea mwanae na kuishinae hapo. Ingawa alikua bado anasoma hakuwa na budi kumsaidia mama yake baadhi ya shughuli ili waweze kupata kipato, siku za kawaida baada ya kurudi shule alikua anakwenda mgahawani kwa mama yake na kumsaidia kazi, alipata usumbufu mwingi kutoka kwa wateja wa kiume ambao mara nyingi walikua wakimtongoza na kumtaka kimapenzi. Kutokana na malezi aliyopewe na heshima aliliokuwa nayo alijitahidi kudharau usumbufu huo ila ulivyoukua unazidi alibidi awe mkali. Mama yake alimsihi asiwe mkali kwa wateja kwani akifanya hivyo watamkimbia mgahawani kwake na ukiangalia tangu yeye arudi wateja wamekua wengi, alimwambia anachotakiwa kufanya ni kuwasikiliza ila asifanye au kukubali watakavyo. Alifanya hiyo ila kadri siku ziendavyo vishawishi vilizidi kuwa vingi shuleni na nyumbani, kwani hata baadhi ya waalimu nao walikua wanamtaka. Akajikuta anahongwa na wateja, wengine kumuachia hela kubwa wakidai ni zawadi. Mary aliangalia maisha ya marafiki zake shuleni wengi wanavaa vizuri na wengine wanamiliki hadi simu. Mary bado akapiga moyo konde na kubaki kwenye mstari.
Siku moja wakati anatoka shule alisikia mlio wa honi ya pikipiki, alipogeuka nyuma alikuta ni teacher wake, teacher alimuomba ampe lifti Mary hakua na shaka kwakua alijua mwalimu anapitaga njia moja ya nyumbani kwao, alipanda pikipiki huku teacher akimpa pole kwa kutembea umbali mrefu. Njiani teacher alimuomba apitie nyumbani kwake kwanza abadili nguo kisha ampeleke mpaka kwao. Mary alikubali, walipofika nyumbani kwa teacher mary alibaki nje Teacher akaingia ndani kubadili nguo, kipindi yupo nje alishangaa anaitwa na teacher aingie ndani, mary alijibu hawezi kwani anaharaka kurudi akamsaidie mama yake, Teacher aliendelea kumuomba aingie ili amsaidie kusahihisha mitihani, Mary aliomba aende anaogopa mama atamgomba kama akichelewa, Teacher alimwambia anamitihani michache tu hivyo amsaidie fasta ili amuwahishe, Mary alimuomba basi aitoe nje ila teacher akamwambia nje watu wakiona watahisi vibaya. Basi Mary akajikuata anakubali, aliingia ndani na kukuta mitihani ipo mezani marry alikaribishwa kwenye kochi akaaanza kusahisha,
Mzee John Charles Kayumba alibarikiwa na Mungu, ujanani mwake Mungu alimbariki akapata mke mwema aitwaye Rose Jamini , wote walikuwa ni wachamungu, kama walivyo wanandoa wengine wa zamani walipitia mengi katika maisha yao ya ndoa shida na raha, lakini walivumilia na mpaka Mungu akawajalia kupata watoto wanne, wakiume watatu na msichana mmoja. (Charles, Emilianna, Makuda na Mussa). Mzee huyo alikuwa ni mtumishi serikalini na mkewe huyo alikuwa ni mama wa nyumbani anayeendesha biashara ndogondogo. Maisha yaliendelea, walilea watoto wao na kuishi kwa furaha sana. Miaka ilipita wakabarikiwa kujenga nyumba tatu, ambapo nyumba moja waliishi wao na watoto wao na nyingine walipangisha.
Siku moja ilikuja kugundulika kuwa mzee huyo alizaa mtoto mwingine nje ya ndoa. Mkewe alihuzunika na kuumia sana, Baada ya mkewe kupata habari hizo kutoka kwa majirani, alifanya uchunguzi na kugundua kuwa habari hizo ni za kweli, na nikweli mzee huyo alizaa mtoto wa kike na mwanamke mwingine. Siku moja baada ya kupata na kukamilisha upelelezi wake na kupata uhakika alimsubiri mumewe na kumuuliza, Mumewe alikiri na kukubali jambo hilo. Jambo hilo lilileta mvurugano kwenye ndoa yao kiasi kwamba ililazimu kuitwa wazazi na ndugu wa pande zote mbili pamoja na viongozi kathaa wa dini ili waje kulisuluhuisha, kikao kilikua kikubwa na kirefu sana ila Mungu ni mkubwa, maana aliwezesha usuluhuisho huo kuwa wa amani na Yule mke kumsamehe mumewe, wageni walioalikwa kwenye kikao hicho waliamuru mume arudi kwenye ndoa na aachane na huyo mwanamke mwingine.
Miezi kadhaa ilipita mke wa Mzee John alimuomba mumewe amlete huyo mtoto aje kukaa nyumbani kwao na kumlea pamoja na wenzake, mzee John alifurahi sana kwani aliona ni jambo bora watoto wake wakikua pamoja wakitambuana na kupendana kama ndugu. Kweli Yule mtoto alikuja nyumbani hapo na kulelewa na mama huyo, Alikua anaitwa Mary, alisomeshwa na kuishi hapo kipindi chote hadi alipomwaliza shule ya msingi, Mungu alimjalia kwani alifaulu mtiani wake na kuendelea na elimu ya sekondali. Kipindi yupo kidato cha pili Mzee John (baba yake) alifariki. Ilikua ni pigo kubwa kwenye familia hiyo, mazishi yalifanyika. Ilipofika siku ya mirathi Mama na Ndugu zake Mary ( dada na kaka zake pamoja na mama yake aliyekuwa anamlea ) walimkataa na kumwambia kuwa hawamtambui, mama mjane alitoa maelezo kwenye kikao hicho kuwa binti huyo alikua ni mfanyakazi wao wa ndani na waliamua kumlea na kumsomesha kama mwanafamiia ila sio mtoto halali wa mwarehemu mumewe na inatakiwa aondoke arudi kwao, Binti Yule hakuamini kinachomtoka kinywani mama yake huyo aliangua kilio na kuuliza kama kunakitu amekosea hadi leo amkatae, alihuzunika sana na kuamua kuondoka na kurudi kwa mama yake mzazi.
Maisha ya mama yake yalikua ya kimaskini sana. Alimpokea mwanae na kuishinae hapo. Ingawa alikua bado anasoma hakuwa na budi kumsaidia mama yake baadhi ya shughuli ili waweze kupata kipato, siku za kawaida baada ya kurudi shule alikua anakwenda mgahawani kwa mama yake na kumsaidia kazi, alipata usumbufu mwingi kutoka kwa wateja wa kiume ambao mara nyingi walikua wakimtongoza na kumtaka kimapenzi. Kutokana na malezi aliyopewe na heshima aliliokuwa nayo alijitahidi kudharau usumbufu huo ila ulivyoukua unazidi alibidi awe mkali. Mama yake alimsihi asiwe mkali kwa wateja kwani akifanya hivyo watamkimbia mgahawani kwake na ukiangalia tangu yeye arudi wateja wamekua wengi, alimwambia anachotakiwa kufanya ni kuwasikiliza ila asifanye au kukubali watakavyo. Alifanya hiyo ila kadri siku ziendavyo vishawishi vilizidi kuwa vingi shuleni na nyumbani, kwani hata baadhi ya waalimu nao walikua wanamtaka. Akajikuta anahongwa na wateja, wengine kumuachia hela kubwa wakidai ni zawadi. Mary aliangalia maisha ya marafiki zake shuleni wengi wanavaa vizuri na wengine wanamiliki hadi simu. Mary bado akapiga moyo konde na kubaki kwenye mstari.
Siku moja wakati anatoka shule alisikia mlio wa honi ya pikipiki, alipogeuka nyuma alikuta ni teacher wake, teacher alimuomba ampe lifti Mary hakua na shaka kwakua alijua mwalimu anapitaga njia moja ya nyumbani kwao, alipanda pikipiki huku teacher akimpa pole kwa kutembea umbali mrefu. Njiani teacher alimuomba apitie nyumbani kwake kwanza abadili nguo kisha ampeleke mpaka kwao. Mary alikubali, walipofika nyumbani kwa teacher mary alibaki nje Teacher akaingia ndani kubadili nguo, kipindi yupo nje alishangaa anaitwa na teacher aingie ndani, mary alijibu hawezi kwani anaharaka kurudi akamsaidie mama yake, Teacher aliendelea kumuomba aingie ili amsaidie kusahihisha mitihani, Mary aliomba aende anaogopa mama atamgomba kama akichelewa, Teacher alimwambia anamitihani michache tu hivyo amsaidie fasta ili amuwahishe, Mary alimuomba basi aitoe nje ila teacher akamwambia nje watu wakiona watahisi vibaya. Basi Mary akajikuata anakubali, aliingia ndani na kukuta mitihani ipo mezani marry alikaribishwa kwenye kochi akaaanza kusahisha,
End of part
one