Saturday, August 19, 2017

JINSI YA KUMSAHAU MPENZI WAKO WA ZAMANI






“Unaweza  kumnunua  binadamu
 lakini  uwezi  kummiliki  binadamu”


Umekuja  duniani  peke  yako,  na  utaondoka  peke  yako  hayo  ndio  maneo  nahisi  wahenga  hawakupaswa  kuyasema  maana  watu  wengi  wanalia  kwa  uwepo wake  maishani  mwetu,  ingawa  ukiangalia  ni  maneno  yenye  ukweli,  maana  ulizaliwa  peke  yako!  lakini  njiani  katika  safari  yako  ya  maisha  ukakutana  na  mtu  (someone  special)  aliyebadilisha  maisha  yako  na  kufanya  jambo   moja  zuri  au  baya  ambalo  ujawahi  kulifanya  maishani  mwako,  UKAMPENDA,  NDIO  ukampenda  na  kumpa  moyo  wako   na  kumfanya  awe  kila  kitu  maishani  mwako   akakufanya  uingie  kwenye  ulimwengu  mpya,   ulimwengu  wa  mapenzi,  ukamkabidhi  moyo  wako  na  ukampa  pendo  lako,  ukashare  nae   busu  lako  la  kwanza,   mwili  wako  kwa  mara  ya  kwanza.   ukajiona  umebarikiwa  kuliko  wanawake/wanaume  wote  duniani.

Muda  ukapita  masaa,  siku,  wiki  miezi  miaka  mkawa  na  furaha  huku  ukiamini  umempata  wa  kufa  na  kuzikana  nae  (the one),  na  ukaamini  hakuna  kitu  kingine  ambacho  ungemuomba  Mungu  akupatie  isipokuwa  muda  wa  furaha  ulionao  na  umpendae.   Kwakua  amekamilisha  maisha  yako 

Lakini  kila  mahusiano  hayakosi  kasoro,  kunakukwazana,  kugombana  na  muda  mwingine  hutumika  maneno  ambayo   hamkusudii  kuyasema,  lakini  kivyovyote   vile   hali  inavyokuwa!  Mlitafuta  njia  na  kusameheana   kama  vile  wapenzi  wa  kweli  wafanyavyo    kusuruhisha  matatizo  yao  na  kurudisha  penzi  lao  kwenye  mstari.  Lakini  yote  hufanyika  na  kuhesabika  na  mwisho  huchukuliwa  kama  malimbikizo  ya  makosa  ambayo  hutoa  hukumu  la  penzi  lenu,  kunasababu  nyingi  za  watu  kutengana  kama  vile   kutovumilia  tabia  zisizo badilika,     kufanya  kosa  lisilosameheka,    lengo lake  limetimia,      kudanganyika  na  watu  wengine,         kushidwa  kuvumilia  hali  ya  kiuchumi  mlionayo,     kupata  mtu  mwingine,     kuona  mpenzi  wako  hana  mipango  ya  baadae  na  wewe,      hakuna  anachokipata  kwako,     wazazi,   kuchokana,     mpenzi  wako  kutoendana  na  hadhi  uliyonayo,      muda  aliyojiwekea  kuwa  kwenye  mahusiano  na  wewe  umeisha,      na  nk       sababu  zipo  nyingi  mno.  Ila  unachotakiwa  ujue  ni  kwamba  sio  kila  anaeingia  kwenye  mahusiano  anakuwa  na  malengo  ya  dhati  na  wewe,     wewe  unaweza  ukawa  kwenye  mapenzi  ila  mwenzio  anapita  tu  kwa  muda,  kivyovyote  vile  inavyokuwa,  bado  kumpoteza  mtu  umpendae  INAUMA.

Sio  wote  wanaoumia  na  mapenzi  wanamapenzi  ya  dhati,  wengine  wanakuwa  wamepoteza  mtu  aliokuwa   ni  msaada  kwao.  ila  asikwambie  mtu  hakuna  kitu  kinachouma zaidi  ya  kumpoteza  mtu  umpendae,  na  hapo  ni  katika  kutumia  lugha  laini  ila  ukweli  ni  kwamba  hakuna  kitu  kinacho  uma  kama  kuachwa  au  kufikia  maamuzi  ya  kuacha.   unajikuta  umejaribu  kila  kitu   kufanya  mahusiano  yaendelee  lakini  mwisho  wa  yote   kunakuwa  hakuna  njia  nyingine  zaidi  ya  kuachana.

Watu  wengi  hupitia  wakati  mgumu  baada  ya  kutengana  na  wapenzi  wao,  mawazo  ndio  pekee  yanayobaki  kwenye  kichwa  chako,  utakumbuka  kila  kitu  mlichokuwa  mnafanya  na  kuomba  umpendae  awepo  mikononi  mwako  wakati  huu  walau  umshike  uhisi  joto  lake  la  mwili  uone  tabasam  lake,  umkumbatie,  umbusu  na  kusikia  yale  maneno  matamu  aliyokuwa  akikwambia,  lakini  inakuwa  kama  ndoto,  maaana  unajikuta  kama  unatoka  usingizini  na  kukutana  na  maumivu  ya  moyo.   ukweli  ni  kwamba  tumeumbwa  tofauti  na  kila  mtu  ananjia  yake  ya  kukabiliana  na  matatizo  aliyonayo.  Kuna  wale  wanao  shindwa  kukubaliana  na  hali  iliyotokea hivyo  kushidwa  kuvumilia  na  kuamua  kuchukua  maamuzi  ya  kukurupuka  na   wengine   kuchukua  maamuzi  ya  kujiua  au  kuhangaika  wajuavyo  ili  wawarudeshe  wawapendao  maishani  mwao,  kuna  wale  wanaoweka  maumivu  yao  moyoni  na  kubaki  wakiumia  ndani  kwa  ndani,  kama  nilivyosema!  kila  mtu  ananjia  yake  ya  kukabiliana.  Kama  unataka  kujua  jinsi  ya  kumsahau  mtu  ulieachana  nae  tafadhali  fuata  hizi  hatua  nitakazo  kuorodhesha  hapa  chini.




MAMBO  YA  KUFANYA


HATUA  YA  KWANZA
PUMZIKA – jipe  muda  wa  kupumzika  usafishe  kichwa  chako  kwani   ni   hali  ya   kawaida  kwa  binadamu  yeyote  kuwa  kwenye  maumivu   uliyonayo.  Kumbuka  wewe  sio  wa  kwanza  na  hautakuwa  wa  mwisho  kukutana  na  jambo  kama  hili.   unatakiwa  kujua  kuwa  wapo  wengi  waliopitia  magumu  zaidi  yako  hivyo  Usifanye  maamuzi  ya  haraka  ambayo  yatakugharimu  baadae.  Usishindane  kuona  wenzako   wapo  kwenye  mahusiano  na  wewe  ukaamua  kurudi   kichwa  kichwa,  chukua  muda  wa  kutosha  huku  unafanya  mambo  mengine.  Zitapita  siku,  wiki,  miezi  hata  miaka  lakini   Mungu  atakujalia  utampata  atakaye  kupenda  kwa   dhati  na  kukufanya  usahau  yote  yaliyopita.

HATUA  YA  PILI
Jisamehe  Usijilaumu -  ingawa  nikawaida  kurudisha  mkanda  nyuma  na  kufikiri  sababu  ya  kipi  kichosababisha  hadi  ukaachana  na  mpenzi  wako,  na  kujikuta   ukijilaumu  kwa  makosa  uliyofanya  au  muda  ulioupoteza   kuwa  naye.  Utafikiria  mengi  mitihani  mliyopitia,  mambo  mliyofanya,   mambo  uliyomfanyia,  ndoto  zenu  mlizo  panga,,  ahadi  mlizowekeana  na  mendine  mengi.  Utakosa  majibu   lakini  inakubidi  ujisamehe  ili  uweze  kuendelea.  Jisamehee,  Uache  moyo  wako  ukiwa  huru.

HATUA  YA  TATU
Msamehe jambo  la  msingi  unalotakiwa  kufahamu  ni  kwamba  daima  makovu    yanatukumbusha  tulipotoka  na  watu  walioyasababisha,  hivyo  basi  ili  kuwa  na  amani  kwa  wakati  ulionao  na  wakati  ujao hunabudi  kumsamehe  mpenzi  wako huyo  wa  zamani  ili  kumtoa  akilini  mwako,  inakupasa  umsamehe  kwani  ukimchukia  utajipa  mawazo  ya  kumfikiria  mara  kwa  mara  na  kumuweka  kichwani  huku  ukiwaza  ya  nyuma (would’ve,  could’ve,  should’ve).  Jambo  ambalo  hastahili  tena  kwako. 

HATUA  YA  NNE
Ondoa  Uwepo  Wake  Katika  Maisha  Yako  Mapya.  Unless  unatatoo  yake  mwilini  mwako!,  Ila  kwa  vitu  vingine  Unapaswa  kushugulikia  kila  kitu  kinacho  kukumbusha  mpenzi  wako  wa  zamani,  rudisha  zawadi  alizokupa,  kusanya  vitu  vyake  vyote  ambavyo  unavyo  viweke  kwenye  mfuko  au  box  kisha  mrudishie  (kwakuwa  uhitaji  kuonana  nae  inakupasa  umpe  mtu  ampelekee)   au  weka  stoo  au  sehemu  yoyote  ambapo  hutaweza  kuviona.  Futa  picha  au  ziweke  kwenye  kifaa ambacho  hutakuja  kukitumia  kwa  muda  mrefu.  Usitupe  na  Usichome  moto  au  kuviharibu  vitu  vyake  uwezi  jua  baadae  vinaweza  kuwa  na  umuhimu  wake  na  utashukuru  hukuvitupa.


Kuna  mazingira  mengine  yatashindikana  kutoa  uwepo  wake  kwako,  kwani   unaweza  kuwa  unasomanae,  mpo  darasa  moja (ni  group  member  mwenzako),   mpo  ofisi  moja,  mnasali  kanisa  moja.  Anaweza  kuwa  ni  bosi  wako  ambaye  kila  siku  unatakiwa  umkabidhi  ripoti, au  mfanyakazi  mwenzako,  mwalimu  wako   na  n.k   ( hii ni  maada  ijayo  utaipata  kwenye  blog  hii  hii  kwenye  machapisho  yajayo  usikose,  stay  tuned)   
 b
HATUA  YA  TANO
hBADILI  MAZINGIRA  (TAKE  A  VACATION/ TRAVEL  AND  CREATE  NEW  MEMORIES  DO  SOMETHING  AWESOME  AND  LOCALLY  AMAZING) -  Kama  ratiba  na  hali  ya  kiuchumi  inakuruhusu  badili mazingira,   ni  vizuri  ukasafiri  ili  kubadili  mazingira  na  kutengeneza  kumbukumbu  mpya,  nenda  sehemu  yeyote   kama  mbuga  za  wanyama,  kawaone  wazazi,  mtembelee  rafiki  yako  kipenzi  aliyembali,  nenda  mji  ambao   hujawai  kufika  (tembelea  sehemu  za  makumbusho,  nenda  viwanja  vya  mipira,  tembelea  vibanda  vya  TV rufufu ila  usiangalie  pilau,  tembelea  maktaba  zilizopo  eneo  hilo)




HATUA  YA  SITA
Badili  ratiba  yako  ya  maisha  ya  kila  siku – usitabirike,  badili  ratiba  yako siku.  Hakuna  akujuae  vizuri  kama  mpenzi  wako  hivyo  ni  wazi  anajua  mwanzo  mwisho  ratiba  yako  na  inakuwa  rahisi  kwake  kujua  cha  kufanya  juu  yako  au  kukutafuta  atakapojisikia,  kama  ratiba  yako  inajulikana  kuwa  ukiamka  asubuhi  saa  4  unakwenda  mgahawani  (your  favourite  dinner) Sio  kwa  kumuogopa  mtu   


HATUA  YA  SABA
BADILI  MWONEKANO  WAKO.  Usionekane  kama  unamajonzi  au  mfiwa,  kuwa  smart,  endelea  kula  vizuri,  vaa  vizuri  tengeneza  nywele  zako  upatapo  muda

HATUA YA  NANE
 TAFUTA  MAHALI  PA  KUWEKA  UPENDO  WAKO.  Kwa  wale  waliobarikiwa  kuwa  na  watoto  (single  parents) inakuwa  rahisi  sana  kwao  kwani  wanaweza  kutumia  muda  wao  mwingi   kuwa  na  watoto  wao  na  kila  maamuzi  watayofanya  yatakuwa  ni  kwa  ajili  ya  manufa  ya  watoto  wao,  tumia  muda  wako  mwingi  kuwa  na  mwanao/wanao  kwani  ndio   watu  muhimu  uliobaki  nao,   mtoto  wako  ni  rafiki  yako,  ni  kipenzi  chako.  Kuwa  mama/baba  bora  kwa  kuhakikisha  mwanao  anapata  malezi  bora  usitetereke.  Msaidie  homework,  Toka  out  katembee  na  mwanao  mpeleke  sehemu  za  makumbusho ,geuka   uwe  mtoto,   ikikubidi  cheza  nae  gorori,  rede  au  mpira,  weka  muda  wa  kukaa  nae  chini  uongee  nae. 

Kama  huna  mtoto  tafuta  paka  au  mbwa.  Ni  bora  kuliko  kukaa  peke  yako   

HATUA  YA   TISA
PANGA  MIPANGO  YA  UCHUMI  YA  SASA  NA  BAADAE ( PLAY  THE  LONG  GAME) -  ili  usitetereke  na  kuendelea  kulaumu  na  kumfikiria  mpenzi  wako  ndio  sababu  ya  kuanguka  kwako  inakubidi  uandae  mipango  endelevu  ya  baadae  ya  maisha  yako,  panga  utakachofanya  kujiingizia  hela  sasa  na  baadae, anzisha  miradi  ya  kukuingizia  fedha  kila  siku, anzisha  miradi  itakayokuingizia  hela  baadae  usichague  kazi.  Kama  huna  mtaji  tafuta  ajira  sehemu  yeyote  usichague  hata  kama  mshahara  ni  mdogo  mradi   utatosha  kuweka  pesa  kidogokidogo  ya  kuanzisha  kitu  unachotaka  kufanya  baadae.

HATUA  YA  KUMI
JITOLEE – tumia  maumivu  yako  kusaidia  watu  wengine  wanao  hitaji  huduma  yao,  watoto  yatima,  wazee  wanaoomba  mitaani.  Fanya  hivyo  na  moyo  wako  utakuwa  na  amani  siku  hadi  siku.

  


HATUA  YA  KUMI  NA  MOJA
USALAMA  WA  UNAPOISHI  hakikisha   mahali  unapo  kaa kuna  usalama  baada  ya  kuchana  mpenzi  wako,  kama  mlikua  mnakaa pamoja  ni  wazi  atakua  anajua  kila  kitu  kuhusu  nyumba  yako  badili  vitasa  au  kufuri  na  uweke  vipya  ili  uwe  na amani.



MAMBO  YA  KUTOFANYA

USIJITENGE  NA  WANAOKUJALI  baadhi  yetu  tumekosa  bahati  ya   kuwa  na  marafiki  lakini  haimaanishi  hatuna  watu  wanaotujali,  mwanzoni  utapenda  kuwa  peke  yako,  utaona  kila  mtu  ni  walewale  lakini  sio  sahihi,  kuna  watu  muhimu  wanaokujali  na  kukupenda  na  daima  watakuwa  karibu  na  wewe  pale  unapowahitaji,  so  usijitenge  nao  kwani  ni  moja  ya  familia  uliyobaki  nayo.

USIGOMBANE  NA  WATU  baada  ya  kuachana  na  mpenzi  wako  ni  dhahiri  maneno  mengi  yataanza  kusemwa  na  kila  mtu  ataongea  lake  ili  mradi  tu.    

USILIPIZE  KISASI   iwe  mmeachana  kwa  heri  au  shari  jitahidi  kutolipiza  kisasi,  najua  utakuwa  na  hasira  utafikiri  mengi  unaweza  ukawa  umebaki  na  picha  za  utupu  za  mpenzi  wako  au  unajua  dili  haramu   alizopiga  zamani ili  kumkomoa  ukaamua  kuweka  hadharani  ili  umuharibie  na  aumie  kama  unavyoumia  wewe .  Jua  kwamba  kufanya  hivyo  utakuwa  umekosea  maana  sio  yeye  tu  atakaye  dharirika  ila  na  wewe  uliesababisha,  na  watu  watakushusha  hadhi  yako  na  kukudharau  kwa  kitendo  ulichokifanya  hata  bila  ya  hayo  nafsi  yako  itakusuta  baadae  na  unaweza  juta  kwanini  ulifanya  hivyo  ndio  maana  wanasema  hasira  hasara.

USITOE  SABABU  ZA  KUACHANA  KWENU  KWA  WATU  BAKI kuachana  na  mpenzi  wako  isiwe  faida  kwa  watu  wengine,  jitahidi  kutosema  ovyo  kwa  watu  sababu  za  kuachana  kwenu.  kumwambia  rafiki  mmoja  au  wawili  unaowaamini  inatosha 

EPUKA  KWENDA  MAENEO  YATAKAYO  KUFANYA  UMKUMBUKE   Kumbukumbu  ndogo  ndogo  zinafanya  tuendelee  kuwashikilia  watu  tuliotengana  nao,  kila  kitu  kina  kumbukumbu  zake  kuanzia  nguo  tunazovaa,  vijiko  tunavyotumia,  nyimbo  tunazo  sikia,  movie  tunazo  angalia,  makochi  tunayokalia,  vitanda  tunavyolalia  na  pamoja  na  sehemu  mbalimbali  tunazotembelea   Jitahidi  kutokwenda  maeneo  ambayo  yatakukumbusha  mpenzi  wako  wa  zamani,  kunauwezekano  mlipenda  kutoka  kila  weekend  na  kwenda  maeneo  mbalimbali  na  mpenzi  wako  huyo,  club,  bar  dinner,  beach,  guest  na  nk.  



EPUKA  ULEVI:  Muhudumu  Ongeza  Glass ndio   wimbo  wa  taifa,  pia  hutumika  na  watu   kama  wewe 
  mliotendwa  na  wapenzi  wenu.  Jambo  la  mwisho  unalotakiwa  kufanya  ni  kunywa  pombe,  na  kuonekana  chizi  mbele  ya  macho  ya  watu.  Ndio  umeachana  na  mpenzi  wako  ila  hiyo  isiwe  sababu  ya  wewe  kuharibu  maisha  yako,  tabia  inajenga  mazoea,  utakapoanza  ulevi  ni  dhahiri  utaendelea  kuwa  mlevi,  maana  pombe  itakuongezea  mawazo  na  sio   kupunguza  pia  utashusha  naendeleo  yako  kwani  pesa  zako  zote  zitaishia  kwenye  pombe.    



EPUKA  MARAFIKI  ZAKE  kama  ulipata  bahati  ya  kutambulishwa  kwa  wazazi  na  marafiki  wa  mpenzi  wako  wa  zamani  inamaanisha  na  yeye  alikupenda  pia,  ila  mambo  yamebadilika  na  imekubidi  mtengane  cha  kufanya  wakati  upo  kwenye  majonzi  ni  kukaa  mbali  na  marafiki  zake  ili  kuepusha  maswali  na  kusikia   habari  zake. 

MITANDAO  YA  KIJAMII jitahidi  kuepuka  mitandao  ya  kijamii,  jua  kuwa  upo  katika  muda  wa  kujiweka  sawa  na  kitu  cha  mwisho  unacho hitaji  kwa  sasa  ni  kukutana  na  habari  zitakazo  kutia  simanzi  au  kuona  picha  ya  mpenzi  wako  wa  zamani  akiwa  na  furaha  na  mtu  mwingine.  Vile  vile  inakubidi  kuepuka  usumbufu  wa  watu  wengine,  Kumbuka  uliposumbuliwa  pindi  upo  kwenye  mitandao  ya  kijamii  (hasa  pale  statues  zako  zilivyokuwa  single)  sasa  kurudi  tena  ni  kama  swala  kukatiza  katika  msitu   wa  simba au  mbwa  mwitu,  bora  simba  unaweza  kukutana  nae  mmoja  akakufaidi  peke  yake,  ila  mbwa  mwitu  wanatabia  ya  kutembea  kikundi  na  ukipita  anga  zao  kila  mmoja  ataondoka  na  kipande  chake.

USIKUBARI  KUWA  NA  URAFIKI NAE  MAPEMA  ni  jambo  la  kwaida  kuendelea  kuwa  na  mahusiano  ya  kirafiki  na  mtu  ambaye  alikuwa  ni  mpenzi  wako  zamani,  ila  inakubidi  ujaribu  kuepukana  naye  kipindi  cha  mwanzoni  baada  ya  kuachana  kwenu  na  kama  yeye  anakujali  hatakusumbua

USIBADILI  TABIA  YAKO kitu  kimoja  inakupasa  ukitambue,  usiruhusu    mtu  akubadilishe  ulivyo  kwa  ajili  ya  furaha  yake. ni  dhairi  utakuwa  umechanganyikiwa  baada  ya  kuachana  na  mpenzi  wako,  utajaribu  kila  njia  ya  kumsahau  katika  hatua  hizo  kunauwezekano  ukabadilika  na  kujipoteza,  nafsi  yako  iliyozoeleka  ikaondoka  na  watu   wanakujali  wakaona  mabadiliko  ambayo  hawakujazoea,  mf  utabadili  tabia  utakuwa  mtu  wa  hasira   na  matusi  wakati  ulikuwa  mpole,  ulikuwa  unakwenda  kuabudu  kanisani  au  msikitini  utakuwa  mtu  wa  viwanja.   Usijione  kwamba  unamapungufu  ndio  maana  mahusiano  yenu  yamevunjika,  jua  kuwa  mpenzi  wako  alikupenda  kwa  tabia  yako,  tabia  uliyokuwa  nayo  kabla  ujakutana  naye  may be  ilikua  nzuri  au  mbaya  ila  kama  familia  yako  walikusifu  basi  haupaswi  kuibadili.

KUANZISHA  MAHUSIANO  MAPYA  ILI  KUMFANYA   X  AWE  NA  WIVU  JUU  YAKO – epuka  kuanzisha  mahusiano  mapya  mapema  na  watu  wengine  kwa  lengo  la  kumfanya  mpenzi  wako  awe  na  wivu,  unaweza  ongeza  tatizo  baada   ya  kupunguza,  vilevile  unaweza  kumuumiza  mtu  unayemtumia  kwani  naye  anaweza  kuwa  na  mapenzi  ya  dhati  juu  yako. Vile  vile  itashusha  thamani  yako.

USIBEMBELEZE -  Kunauwezekano  makosa  yalikuwa  yako  au  yake  ila  kabla  ya  kuachana  kwenu   ulijitahidi  kufanya  kila  kinachowezekana  kuhakikisha  mmbo  yenu  hayazidi  kuwa  mabaya,  ukatafuta  wasuruhishi  ukabembeleza, na  kubembeleza,  na  kuzidi  kubembeleza,  lakini  jitihada  zako  hazikuzaa  matunda.  Nakushauri  usiendelee  kubembeleza  tena  baada  ya  kuachana,  maana  kufanya  hivyo  utakuwa  mtumwa  na  utaendelea  kujidharirisha  na  kushusha  hadhi  yako  zaidi  na  kumpa  kichwa  mpenzi  wako  na   atakuona   kuwa  huwezi  kuendelea  bila  yeye,  na  utakuwa  unamkufuru  Mungu.  Inakubidi  utambue  kuwa  ulifanya  kila  kinachowezekana  lakini  ikashindikana.

USITIE  HURUMA – usiwe  katika  hali  ya  kuwa  mnyonge  kupitiliza  ili  watu  wakuone  na kuamini  watapeleka  ujumbe  kwa  mpenzi  wako  ili  mrudiane.  Jua  swala  hilo  linaweza  kufanya  kazi  au  likafeli  na  kujikuta  unaendelea  kujidharirisha  tu  mbele  yake  na  kwa  watu  wakuzungukao.

TOA  MATUMAINI  YA  KURUDIANA  NAE  usiwe  na  imani  ya  kwamba  aendapo  atakosa  mtu  mwingine  atakayempenda  kama  wewe  ulivyo  mpenda  au  yatamkuta  mabaya  na  atarudi  tena  kwako.  Jua  kuwa  Uwezekano  huo  upo  na  uwezekano  huo  haupo  maana  “dua  la  kuku  halimpati  mwewe”.  Kuwa  na  imani  hiyo  kutakufanya  wewe  usiendelee  na  maisha  yako  huku  muda  ukienda,  mwenzio  atapata  mtu  mwingine   atakaye  mpenda  zaidi  yako, ataanzisha  familia,  hata  kama  itatokea  akaachana  nae  kunauwezekano  asirudi  kwako  atatafuta  mtu  mwingine    wakati   huku  wewe  ukiendelea  kusubiri.  Na  kama  atarudi,  atarudi  kipindi  amechoka,  katumiwa  hadi  kaisha  hana  mtu  mwingine  anaye  mtaka  ndio  anarudi  kwako  (nikawaida  ya  binadamu,  tunapopata  matatizo  tunakumbuka  tulipotoka  na  watu  waliokuwa  wanatujali  kipindi  hatuna  kitu,  baada  ya  kupata  tunasahau  yote  na  kuwaacha  wapendwa  wao  nyuma)   Unachotakiwa  kufanya  fanya  mambo  yako  akitokea  mtu  atakaye  dhihirisha  upendo  wake  kwako  fungua  moyo  wako  mpende   usimfananishe  na  mpenzi  wako  wa  zamani  jua  kuwa umeanza  ukrasa  mpya  (I  know  how  it  feels,  I  know  its  hard  to  fall in  love  again  for  people  who  truly   loved  once.  Someone  will  come  around ,  when  then  do …. don’t  replace  them,  just  start  over)   lakini  hakikisha  umesamehe  na  usiwe  na  imani  ya  kurudiana   ila  muombee  apate  mtu  atakaye  mpenda  na  kumthamini  zaidi  ya  wewe  ulivyompenda  na  kumthamini  fanya  hivyo  ili  baadae  asije  kukusumbua  na  kukukumbusha  machungu  uliyoyasahau.


MAMBO  YA  KUJIANDAA

MASWALI  -  marafiki  wataona  mabadiliko  pamoja  na  wanafki  pia,  wote  wanojua  na  wasiojua  watakuuliza  maswali  ili  kujua  kwa  undani  sababu  za  kutengana  kwenu.  Hivyo  unatakiwa  kujiandaa na  maswali  hayo.  Kweli  hayawahusu  ila  hutakiwi  kuonesha  hasira. 

KUKUTANA  NAE:  milima  haikutani  binadamu  wanakutana,  baada  ya  kuachana  jua  kwamba  ipo  siku  unaweza  kukutana  na  mpenzi  wako  wa  zamani.  Usioneshe  kukasirika  ukionana  nae  itikia  salamu  kama  atakusalimia  kisha  endelea  na  mambo  yako,  hakuna  haya  ya  kupeana  namba  au  kujua  nini  unachofanya.  Kumbuka  hujabadilika,  wewe  ni  Yule Yule  alie  kuacha  na  ni  Yule  Yule  anaekuona  wa  maana  sasa.

KUTAFUTWA   baada  ya  kuachana  na  mpenzi  wako  jua  kwamba  mbele  ya  safari  lazima atakutafuta,  usishangae  kuona  friend  request kwenye  FB  au  namba  ngeni  inakupigia  na  kujitambulisha  kuwa  yeye  ni   x  wako, 

KUTONGOZWA,  ulipokuwa  kwenye  mahusiano  watu  walikutaka  na  unapotoka  kwenye  mahusiano  usishangae  hata  mashemeji  zako  wakaomba  mzigo,  ndio!  Hilo  ndio  neon  linalotumika  kwa  sasa.  

KUTISHWA,  muda  utapita  na  wewe  utaendelea  na  maisha  yako,  ila  baadae  mpenzi  wako  anaweza  kutaka  kurudiana  na  wewe,  anajua  udhaifu  wako  ataanza  kwa  upole  na  kukukumbusha  mambo  ya  nyuma  na  jinsi  mlivyokuwa  na  furaha  utakapo  mkatalia  usishangae  kupata  vitisho  toka  kwake.



MAMBO  YA  KUKABILIANA  NAYO
 UPWEKE – kuna  uwezekano  mkubwa  ukawa  pekeyako  katika  kipindi  hicho  chote ,  ulishazoea  kulala  na  mpenzi  wako  sasa  upo  pekeyako  kitandani, unamiss  hata  mabishano  mliokuwa  mnabishana. Usijali!  Itakuwa  vigumu  mwanzoni  lakini  badae  utazoea  na  utakuwa  sawa



MIKASI – inawezekana  ulishazoea  siku  kutopita  bila  kupata  morning  kiss,  au  yale  mavituz   ambayo  yalikufanya  uone  raha  za  dunia,  ulishazoea  kusumbuliwa  wakati  umechoka,ulishazoea  kunyonya  mandingo  ya  mpenzi  wako  kila  wakati,  ulizoea  kutomaswa,  ulizoea   kukunjwa,  kuinamishwa,  kuchuma  matembele,  kupiga  kelele  hadi  majirani  wanaona  kero,  sasa  kaondoka  umebaki  peke  yako  na  kitanda  unakiona  kikubwa,  unalala  na  mdori  ukiukumbatia  kwa  nguvu  lakini  kwa  bahati  mbaya  mdoli  wako  haiung’ati,  “I  don’t  want to  turn  you  on”  cz  upo  sad  unalala  peke  yako,  unaamka  peke  yako.  lakini  unatakiwa  kuwa  jasiri   jitahidi  kujishughulisha  na  mambo  mengine  fanya  kazi  ili  akili  yako  ichoke,  uondoe  mawazo  hayo.  Jiunge  na  gym  au  anza  ratiba  ya  kufanya  mazoezi  itakusa  kuondoa  tama  za  mwili.
  





Cha  kuzingatia:. 

 Mara  nyingi  inapotokea  jambo  kama  hili  la  kutedwa  watu  wengi  hutupia  lawama  kwa  jamii  ya  mtu  aliemtenda.  Mf  wanaume  huwaita  wanawake  Malaya  kwasababu  tu  aliachwa  au  alimuacha  mwanamke  aliymkosea.  wanawake  nao  hivyo  hivyo  huwaita  wanaume  walewale  kwasababu  ya  kutendwa  na  mtu  mmoja.  Kiukweli  jambo  hili  sio  sawa,  sababu  zinazofanya  uchukue  imani  hizo  ni  kwamba  baada  ya  kutendwa  ulikurupuka  bila  kupumzika  na  kuanza  mausiano  mapya  na  watu  wengine  bila  kufikiria  ili  tu  uweze  kupunguza  maumivu  uliokuwa  nayo,  kuogopa  upweke   au  ulitaka  kulipiza  kisasi  kwa  kutembea  na  rafiki  yake  au  akuone  utetereki  kwa  kuwa  upo  na  mtu  mwingine (kata  mti  panda  mti, ukishuka  wenzio  wanapanda,  ukisema  cha  nini …….. na  nk),  hata  hivyo  mtu  huyo  uliekuwa  unamtumia  hukuweza  kuendelea  nae  kwakuwa  ulijilazimisha  kuwa  naye.


      kama  nilivyosema  mwanzo  sio  kila  mtu  anaeingia  kwenye  mahusiano  anakuwa  na  malengo  ya  dhati  sio  kwamba  kila  anaeingia  kwenye  mahusiano  anamalengo  mabaya,  mapenzi  ya  mapenzi  ya  kweli  yapo
Muda  utapita  vidonda  vitapona,  utasahau
Atatokea  mwingine  anaweza  kuwa  mbaya kuliko  mpenzi  wako  wa  zamani
Au  anaweza  kuwa  bora  zaidi  ya mpenzi  wako  wa  zamani

Maisha  yanaendelea

USIPANGE  KUWA  NA  MALAIKA.  Jua  kabisa  hali  hii haitakuwa  ya  kudumu  ipo  siku  utapata  mtu  mwingine.  Tatizo  tulilonalo  binadamu  ni   kwamba  ikitokea  mtu  amepatwa  na  mkasa  kama  huu  atajitahidi  kutafuta  mtu  ambaye  ni  mzuri  zaidi  ya  Yule  aliyeachana  nae.  Jambo  ambalo  litakufanya  uendelee  kutumika  maana   utategemea  kuwa  umepata   malaika  kumbe  umeangukia  mikononi  mwa  shetani  matokeo  yake  ni  moto  kila  siku  ndani




Next  topic



HOW  DO  TO  FIND  TRUE  LOVE

Mapenzi  ya  kweli  hayachagui,    Awe  mzuri,  mbaya,  hana  elimu  lakini  ana  mapenzi  ya  kweli.  je  utamkataa  kwasabau  Hana  cha  kukupa  zaidi  ya  mapenzi  aliyonayo.  Haijalishi  watu  wengine  wanamuonaje  (marafiki/ wazazi)  kinachojalisha  ni  furaha  yako  wewe  na  yeye.  Muda  ukifika  wataelewa.




3 comments:

  1. Jina langu ni Ago, kutoka Albania. Nitapenda kushiriki uzoefu wangu juu ya jinsi ninavyopona mpenzi wangu mzuri kutoka kwa mnyang'anyi wa mke
    Nilipoteza rafiki yangu wa kike safi na mzuri kwa mtu mwingine. Nilikuwa na huzuni na nilitaka arudi vibaya tena. Nilikuwa nikimpigia Dk.Sango kwa usomaji na ushauri na nikagundua atanisaidia. Uchawi wake wa upatanisho ulimrudisha mpenzi wangu mpendwa. alisahau kabisa juu ya yule mtu mwingine na alirudi kwangu akiwa wazi na mwenye upendo kama hapo awali. Sasa wasiliana na daktari, Dk Sango, ikiwa unahitaji kushauri juu ya uhusiano wako au aina yoyote ya shida kwenye barua pepe yake. inaelezea mtaalam937@gmail.com

    ReplyDelete
  2. Nilikuwa kwenye hatihati ya kumpoteza mke wangu wa miaka sita kwa sababu alisema hakuwa na hamu tena na ndoa yetu, ambayo inalea binti mzuri kwa sababu kama dereva wa lori huwa nikienda barabarani, lakini nampenda sana na namjali mke wangu. Nilimuuliza yeye na binti yangu shida ni nini, lakini hakutoa ufafanuzi mzuri, akisema alikuwa amechoka na umoja wetu, ilikuwa ya ajabu kwangu kwa sababu mke wangu alikuwa mwanamke mwenye upendo, ghafla kila kitu hubadilika tu. na mtazamo wake kwangu haukuwa mzuri, nilijua ilikuwa mbaya mahali pengine, kwa hivyo nilielezea mambo kwa rafiki yangu mzuri Micheal, ambaye alinitambulisha kwa jina la mwandishi wa spell Dr.Pellar, nilielezea hali yangu kwa mwandishi, ilifanya ninatambua kuwa mpenzi wa zamani alikuwa akimdanganya mke wangu kuniacha, lakini akaniambia nisiwe na wasiwasi. Nilifuata maagizo yote na mke wangu alirudi kwa ustawi wake wa kawaida na ninashukuru sana kwa kile msaidizi wa Dr.Pellar amenifanyia, kwa hivyo nashiriki shuhuda zangu ikiwa unakabiliwa na shida yoyote maishani na unahitaji suluhisho kuwasiliana na daktari huko DrPellar kwenye barua pepe yake drpelar@gmail.com

    ReplyDelete
  3. Nilikuwa kwenye hatihati ya kumpoteza mke wangu wa miaka sita kwa sababu alisema hakuwa na hamu tena na ndoa yetu, ambayo inalea binti mzuri kwa sababu kama dereva wa lori huwa nikienda barabarani, lakini nampenda sana na namjali mke wangu. Nilimuuliza yeye na binti yangu shida ni nini, lakini hakutoa ufafanuzi mzuri, akisema alikuwa amechoka na umoja wetu, ilikuwa ya ajabu kwangu kwa sababu mke wangu alikuwa mwanamke mwenye upendo, ghafla kila kitu hubadilika tu. na mtazamo wake kwangu haukuwa mzuri, nilijua ilikuwa mbaya mahali pengine, kwa hivyo nilielezea mambo kwa rafiki yangu mzuri Micheal, ambaye alinitambulisha kwa jina la mwandishi wa spell Dr.Pellar, nilielezea hali yangu kwa mwandishi, ilifanya ninatambua kuwa mpenzi wa zamani alikuwa akimdanganya mke wangu kuniacha, lakini akaniambia nisiwe na wasiwasi. Nilifuata maagizo yote na mke wangu alirudi kwa ustawi wake wa kawaida na ninafurahi sana kwa kile msaidizi wa DrPellar amenifanyia, kwa hivyo nashiriki shuhuda zangu ikiwa unakabiliwa na shida yoyote maishani na unahitaji suluhisho kuwasiliana na daktari huko DrPellar kwenye barua pepe yake drpellar@gmail.com

    ReplyDelete

MASWALI YANAYOWEZA KUULIZWA KWENYE INTERVIEW YA TRA MARCH 2025

  ANGALIZO Haya ni baadhi ya mawaswali  ambayo yanaweza yakatoka au yasitoke kutokana na ajira ulioiomba, hiyo unatakiwa kuyapitia na kuso...